Breaking News

FAMILIA YA MEJA KUNTA YADAI HAWANA TAARIFA RASMI ZA KIFO CHA MTOTO WAO

Redio ya EFm wametoa taarifa kwamba mpaka sasa hawana taarifa rasmi kama kweli Meja Kunja amefariki dunia ingawa ni kweli alipata ajali Tanga wakati anaelekea kwenye Tamasha la Muziki Mnene.

Hiii ni taarifa rasmi ya EFm ambao walikuwa karibu na Meja Kunja. “KUHUSU MEJA KUNTA.

MejaKunta alipata ajali jana akiwa anaenda Tanga kwenye #MzikiMnene, tamasha ambalo tunaliandaa sisi (@efmtanzania na @tvetanzania)
.
Tulifanya kila lililo ndani ya uwezo wetu, kushirikiana na watu wake wa karibu pamoja na Madaktari kuhakikisha anapona.

Hadi kufikia leo mchana, tulikuwa tunafuatilia kwa karibu maendeleo yake. Tayari aliondoka Tanga kurudi Dar es Salaam tukijulishwa kwamba anaendelea vizuri.

Usiku huu tumepokea taarifa za kifo chake, kama zinavyosambaa katika vyombo mbalimbali zikielezwa kuwa zimetoka kwa meneja wake (#GMaker). Sisi kwa haraka tulikwenda nyumbani kwao Temeke, bahati mbaya huku nako hakuna anayeweza kuthibitisha taarifa hizo (Iwapo Meja Kunta amefariki ama ni Mzima). Ndugu hawana taarifa rasmi. #GMaker pamoja na watu wengine wa karibu, hawajapatikana kuthibitisha taarifa hizi.
.
Tunaomba uvumilivu, tuko pamoja na familia ya Mejja Kunta na wahusika wote ili kufahamu undani wa suala hili. Tutatoa taarifa rasmi juu ya chochote kitakachothibitika.
.
Asanteni”


isikilize hapa 

No comments